Skip to main content
  • Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Aipongeza Kanda ya MSD Tanga kwa Kuvuka Malengo ya Mauzo

    Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) Dkt. Rukia Mwifunyi amepongeza Kanda ya MSD Tanga kwa kuvuka malengo ya mauzo, katika robo mwaka ya kwanza ya mwaka kwa asilimia 12.

    Mjumbe huyo wa Bodi, ambaye ni mlezi wa Kanda ya MSD TANGA amefuatana na  Meneja Huduma za Sheria MSD, Elisamehe Macha katika ziara ya kutembelea wateja wanaohudumiwa na Kanda ya Tanga,ziara ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka thelathini (30) ya utendaji wa MSD tangu kuundwa kwake.

  • MSD Yapongezwa kwa Mabadiliko na Maboresho ya Kiutendaji Katika Kipindi cha Miaka 30

    Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Dkt. Elisha Robert Ndaki ameipongeza Bohari ya Dawa(MSD) kwa kuboresha huduma kwa wateja, sambamba na upatikanaji wa bidhaa za afya kwa wakati, hali iliyowezesha kupungua kwa malalaiko ya wateja na wananchi kwa ujumla.

    Dkt. Ndaki ametoa pongezi hizo hii leo tarehe 21/11/2024 mbele ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Bw. Ally Seleman wakati ujumbe kutoka MSD ulipotembelea kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya Shinyanga.

  • MSD YASHINDA TUZO TATU ZA MWAJIRI BORA 2024

    Bohari ya Dawa (MSD) imejinyakulia tuzo tatu za Mwajiri bora mwaka 2024 kupitia tuzo zinazotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE).

    Katika tuzo hizo zilizotolewa na Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Biteko, MSD imeibuka na ushindi wa tuzo tatu ambazo ni pamoja na Taasisi bora kiutendaji (Club of Ten best performers), mshindi wa kwanza kwa taasisi inayotoa fursa za ajira (First runner up job creation na mshindi wa pili Mwajiri bora sekta ya umma (Second runner up Public Sector).

  • Mkoa wa Dodoma Wajipanga Kuboresha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya

    Meneja MSD Kanda ya Dodoma Bi. Mwanashehe Jumaa ameuomba uongozi wa Timu ya Usiamizi wa afya Mkoa wa Dodoma (RHMT) kuratibu na kusimamia uwasilishwaji wa maombi ya mahitaji ya  vituo vya kutolea huduma za afya kwa wakati na ulipaji wa madeni, ili MSD iendelee kutoa huduma kwa ufanisi na kwa wakati.

  • Bohari ya Dawa (MSD) Kukuza Ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

    Bohari ya Dawa (MSD) imekutana ujumbe kutoka  Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) lengo likiwa kuanzisha ushrikiano wa kiutendaji kwenye nyanja za Utafiti, Ubunifu, Teknolojia, TEHAMA, Biashara na Fedha. Kikao hiko cha ushirikiano kimefanyika Makao Makuu ya MSD Keko Dar es Salaam,  huku kikikutanisha maafisa mbalimbali kutoka kwenye taasisi hizo. 

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.