Ruka kwenda maudhui makuu

Kitengo cha Miradi Misonge

Kitengo cha Miradi Msonge cha  Bohari ya Dawa (MSD) ni kiini cha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya nchini Tanzania, kikihakikisha uratibu na upatikanaji wa bidhaa za afya kwa ajili ya program za  VVU/UKIMWI, Kifua Kikuu, Malaria, Chanjo, na Afya ya Uzazi na Mtoto.


Hapo kabla, programu hizi zilikuwa zikiendeshwa bila kushirikiana chini ya Wizara ya Afya, kila programu iliendesha mfumo wake wa ugavi, na kusababisha  kukosa ufanisi na kuwa na matumizi ya rasilimali yasiyo na tija. Mwaka 1996, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliunganisha shughuli zote za ugavi  kuwa chini ya MSD ili kurahisisha utendaji kazi, kupunguza gharama, na kuimarisha uwajibikaji katika mnyororo wa ugavi.


Kitengo hiki kinasimamia ununuzi, uhifadhi, na usambazaji wa bidhaa za programu kwa kushirikiana kwa karibu na wabia wakubwa wa maendeleo kama vile Mfuko wa Dunia, UNICEF, Shirika la Afya Duniani, na USAID. Ushirikiano wa programu unahakikisha  bidhaa zinazogharamiwa  na wahisani zinatolewa kwa wakati, uwazi, na kwa ufanisi katika vituo vya kutolea huduma za afya nchi nzima.


Kupitia uratibu thabiti, mifumo iliyounganishwa na kuzingatia viwango vya ubora, Kitengo cha Miradi Msonge za kinatekeleza  dhamira ya MSD ya kuhakikisha kunakuwa na mnyororo wa ugavi bora, wenye ufanisi, kuamika na endelevu wa bidhaa za afya za miradi msonge nchini Tanzania.
 

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.