Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini
Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini pia hujulikana kama Ofisi ya Usimamizi wa Kimkakati ni kitovu cha maarifa cha MSD kinachojishugulisha na uchanganuzi wa utendaji kazi, utekelezaji wa Mpango mkakati , ubunifu kupitia uchanganuzi wa taarifa, udhibiti wa vihatarishi na kufanya tathmini utekelezaji wa majukumu ya MSD.
Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini, kama kitovu cha maarifa cha taasisi huakikisha malengo, shughuli na rasilimali za MSD zinaendana na vipaumbele na malengo ya MSD ya muda mrefu. Kitengo hiki huratibu uandaaji na utekelezaji wa Mpango Mkakati, kufuatilia utekelezaji wake, utendaji kazi wa taasisi kwa kutumia viashirio muhimu vya utendaji na kuipatia menejimenti taarifa ya kitaalamu inayowezesha kufanya uamuzi sahihi.
Pia, Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini huratibu shughuli za utafiti, uchanganuzi wa uwekezaji na tathmini ya vihatarishi ili kuhakikisha mpango mkakati unasimamiwa na kutekelezwa kwa ufanishi. Kitengo hiki kina watalaamu mbalimbali kama vile wafamasia, wachanganuzi wa masuala ya fedha, wabobezi wa masuala ya mnyororo wa ugavi, watakwimu, wachumi, na wachanganuzi wa vihatarishi ambao kwa pamoja huisaidia taasisi kutoa huduma bora na matokeo yanayopimika katika utekelezaji wa shughuli zake.
Kwa kusimamia utamaduni wa utendaji kazi na uwajibikaji, Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini huimarisha ufanisi, utawala bora, na ustahimilivu. Uongozi na utendaji wake wa ufuatiliaji wa kimkakati na tathmini huhakikisha MSD inaendelea kutoa huduma bora, endelevu na za uhakika za mnyoro wa ugavi wa bidhaa za afya nchi nzima.