Skip to main content
Health Product Manufacturers From the Czech Republic Visit MSD

Wazalishaji Bidhaa za Afya Kutoka Jamhuri ya Ucheki, Waitembelea MSD

Wajumbe wa chama cha viwanda vya kuzalisha bidhaa za afya kutoka Jamhuri ya Ucheki (Czech) ambao wako ziarani nchini Tanzania wametembelea Bohari ya Dawa (MSD) na kuelezea maeneo mbalimbali wanayoweza kushirikiana na Tanzania hasa upande wa bidhaa afya.

Wajumbe hao ambao wamefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye pia anahusika na Jamhuri ya Ucheki (Czech) Dkt. Abdallah Possi wameeleza kuwa ziara yao nchini Tanzania ina lengo pia la kuimarisha mahusiano ya kidoplamasia na kuangalia maeneo ya ushirikiano upande wa bidhaa za Afya ambazo ni pamoja na dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara.

Kwa mujibu wa Rais wa Chama hicho Petr Foit, idadi kubwaya viwanda nchini mwao imejikita zaidi kuzalisha bidhaa za afya, hivyo ni vyema wakajua Tanzania ina uhitaji wa bidhaa za aina gani ili kuweza kushirikiana katika hilo.

Ujio huo pia umeonesha nia ya kuipatia Tanzania bidhaa za kujikinga na magonjwa ya mlipuko ikiwa ni pamoja na Ebola, ambapo Wizara ya Afya kupitia MSD watakaa na kuainisha mahitaji hayo,na kuwasilisha kwa Rais wa Umoja huo wa wazalishaji ili kufanya utaratibu wa kupata bidhaa walizonazo.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.