Skip to main content
  • Somalia Kushirikiana na MSD, Ununuzi wa Bidhaa za Afya

    Rais wa Somalia Mheshimiwa Hassan Sheikh Mohamud amesema nchi yake imeamua kushirikiana kwa karibu na Bohari ya Dawa ya Tanzania katika ununuzi wa bidhaa za afya na kubadilishana uzoefu wa namna mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya unavyofanya kazi.

    Rais Mahamud ambaye yuko ziarani nchini Tanzania, ameyasema hayo alipoitembelea MSD, na kuongeza kuwa kutokana na uzoefu wa MSD, wana uhakika kuwa ubora wa bidhaa za afya utakuwa wa uhakika.

  • Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aipongeza MSD kwa Maboresho ya Huduma

    Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameupongeza uongozi wa Bohari ya Dawa (MSD) kwa mabadiliko makubwa yanayoendelea katika taasisi hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa yamewezesha kupunguza malalamiko ya uhaba wa bidhaa za afya nchini, mathalani malalamiko ya uhaba wa dawa.

    Mhe. Senyamule ameeleza kwamba awali wakienda kwenye mikutano ya hadhara kuongea na wananchi, walikumbana na malalamiko mengi ya uhaba wa dawa, lakini hivi karibuni hali imebadilika, japokuwa bado kuna changamoto, lakini angalau inatia moyo kuona kuna mageuzi yanafanyika.

  • MSD kusambaza vidonge mil 22 vya vitamini A nchini

    Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameikabidhi Serikali ya Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu vidonge milion 22  vya matone vya Vitamini A kwa ajili ya watoto, vilivyotolewa na serikali ya Canada, kupitia shirika la Nutrition International (NI). 

    Dkt. Kikwete, amekabidhi dawa hizo akiwa mmoja wa wajumbe wa bodi wa Shirika la kimataifa la Nutrition international ambalo ndio limetoa msaada huo. 

  • MSD Yakutana na Wataalamu wa Maabara Nchini

    Bohari ya Dawa (MSD), imekutana na wataalam wa maabara ambao ni Mameneja wa maabara za hospitali za Rufaa za Mikoa,Maalum,Kanda na Taifa. Kikao hiki kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Dar es Salaam lengo lake ni kutathimini upatikanaji na ubora wa bidhaa za afya za maabara zinazosambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini. 

    Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, amewaeleza washiriki kuwa watumie siku hizi tatu zilizopangwa kuhakikisha wanakuja na majawabu ya changamoto zinazojitokeza katika sekta hii ya maabara. 

  • Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na UKIMWI Yaridhishwa na Utendaji wa MSD.

    Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imesema  imeridhishwa na hali ya utendaji wa Bohari ya Dawa(MSD) na mipango ya utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo uzalishaji wa dawa ili kupunguza kununua dawa nje ya nchi. 

    Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stansilaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya hali ya utendaji na majukumu ya Bohari ya Dawa (MSD), ambapo ameichagiza MSD kuongeza ufanisi, ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha bidhaa za afya zinakuwa toshelevu na  kusambazwa.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.