Skip to main content
  • MSD Yaanza Usambazaji wa Vifaa Tiba kwa Majimbo ya Mkoa wa Morogoro

    BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza usambazaji majimboni vifaa  tiba  vilivyonunuliwa na serikali vyenye  thamani ya zaidi ya Sh bilioni 14.9 kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati  lengo ni kupunguza vifo vya mama na mtoto.

    Meneja wa MSD, Kanda ya Dar es salaam, inayohudumia mikoa ya  Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Visiwa vya Zanzibar, Betia Kaema alisema hayo wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Adam Malima kwa ajili ya majimbo 11 ya Mkoa huo.

  • Rais Samia Atoa Vifaa Tiba vya Mil. 691 Kwa Majimbo 10 - Dar es Salaam

    RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hususani huduma ya mama na mtoto lengo likiwa ni kupunguza vifo vitonavyo na uzazi pingamizi.

    Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alipokuwa akiwakabidhi wabunge wa majimbo 10 ya mkoa wa Dar es Salaam, vifaa tiba vyenye thamani ya sh. Milioni 691 vilovyotolewa na serikali kwa majimbo hayo.

  • Waziri Ummy Azindua Usambazaji wa Vifaa Tiba vya Huduma za Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto

    Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu azindua usambazaji wa vifaa vya kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto vya zaidi ya sh.bilioni 14.9 ambavyo vitasambazwa katika majimbo 214 na halmashauri nchi nzima.

    Akizungumza jijini Dar es Salaam Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa uzinduzi huo, Waziri Ummy alisema uzinduzi wa usambazaji wa vifaa vya hivyo umelenga kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto na kuimarisha uzazi salama nchini.

  • Katibu Mkuu Afya, Aitaka MSD Kuwajali Wateja Wake

    Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. John Jingu ameilekeza Bohari ya Dawa (MSD) kuwajali wateja na kuwashirikisha katika suala zima la kuwapa huduma za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za Afya nchini.

    Dkt. Jingu amesema hayo wakati  akifungua kikao cha ishirini na mbili  (22) cha baraza la Wafanyakazi la MSD Mkoani Morogoro ambapo amesisitiza kuwa, kujali wateja ni msingi wa kuwahudumia kulingana na mahitaji yao.

  • MSD Yakabidhi Vifaa Tiba vya Mil. 114 - Kituo cha Afya Mtae

    SERIKALI imetoa Sh.Milioni 114 kwa Kituo cha Afya  Mtae kilichopo Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ambazo zimetumika kununulia vifaa tiba kupitia Bohari ya Dawa (MSD) na hivyo kinatarajia kuanza kutoa huduma ya upasuaji mwishoni mwa mwezi Disemba 2023.

    Hatua ya kituo hicho kuanza  kutoa huduma hiyo inatokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya kuibadilisha zahanati ya kijiji cha Mtae kuwa Kituo cha  Afya ili wananchi waweze kupata huduma bora na karibu.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.