Skip to main content
  • MSD YAKABIDHI JENERETA LA KVA 75 KWA HOSPITALI YA WILAYA YA KITETO

    Hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto mkoani Manyara imeondokana na changamoto ya kukatiza baadhi ya huduma za matibabu kama upasuaji na pindi umeme unapokatika baada ya Bohari kuu ya dawa MSD kukabidhi jenereta lenye thamani ya shilingi milioni 65 itakayotumika kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano mjini Kibaya wilayani Kiteto, meneja wa MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema jenereta hilo lenye uwezo wa KVA 75 ni sehemu ya mahitaji ya vifaa vya afya vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 699 vilivyoagizwa na hospita

  • MSD Kusambaza Vyandarua Milioni.1.55 Mkoa wa Shinyanga

    Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) inatarajia kusambaza jumla ya vyandarua milioni moja na nusu, kwa wananchi katika ngazi ya kaya Mkoani  Shinyanga, ikiwa ni kampeni maalum yenye lengo la kupambana na kutokomeza ugonjwa wa malaria nchini.

    Hayo yameelezwa leo februari 8,2025 na Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD Bw.Victor Sungusia, wakati wa uzinduzi zoezi la kusambaza vyandarua mkoani humo, kupitia kampeni maalum  (TMC) chini ya mpango wa taifa wa kudhibiti malaria nchini(NMCP).

  • Waziri Jenista Mhagama Apongeza Mradi wa Ujenzi wa Ghala la Kisasa la MSD-Dodoma

    Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama February 6, 2025 ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma, na kupongeza hatua za maendeleo ya mradi huo wa kimkakati ambao umefikia. asilimia 85%.

  • Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana

    Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana kwa karibu ili kihakikisha wanaendelea kuboresha upatikanaji wa bidhaa  za afya nchini na kuwa utaratibu wa kulipa madeni ili kuiwezesha MSD kuwa na mtaji mzuri wa kuendelea kununua bidhaa za afya.

  • Wizara ya Afya Somalia, Yaja Kujifunza MSD na Kubadilishana Uzoefu

    Wizara ya Afya nchini Somalia imeichagua  Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kushirikiana kwenye masuala mbalimbali yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya kwa  kubadilishana uzoefu katika maeneo ya mifumo, ununuzi, usambazaji na udhibiti ubora.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.