MSD Kusambaza Vyandarua Milioni.1.55 Mkoa wa Shinyanga
Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) inatarajia kusambaza jumla ya vyandarua milioni moja na nusu, kwa wananchi katika ngazi ya kaya Mkoani Shinyanga, ikiwa ni kampeni maalum yenye lengo la kupambana na kutokomeza ugonjwa wa malaria nchini.
Hayo yameelezwa leo februari 8,2025 na Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD Bw.Victor Sungusia, wakati wa uzinduzi zoezi la kusambaza vyandarua mkoani humo, kupitia kampeni maalum (TMC) chini ya mpango wa taifa wa kudhibiti malaria nchini(NMCP).