Skip to main content
  • MSD Kusambaza Vyandarua Milioni.1.55 Mkoa wa Shinyanga

    Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) inatarajia kusambaza jumla ya vyandarua milioni moja na nusu, kwa wananchi katika ngazi ya kaya Mkoani  Shinyanga, ikiwa ni kampeni maalum yenye lengo la kupambana na kutokomeza ugonjwa wa malaria nchini.

    Hayo yameelezwa leo februari 8,2025 na Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD Bw.Victor Sungusia, wakati wa uzinduzi zoezi la kusambaza vyandarua mkoani humo, kupitia kampeni maalum  (TMC) chini ya mpango wa taifa wa kudhibiti malaria nchini(NMCP).

  • Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana

    Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana kwa karibu ili kihakikisha wanaendelea kuboresha upatikanaji wa bidhaa  za afya nchini na kuwa utaratibu wa kulipa madeni ili kuiwezesha MSD kuwa na mtaji mzuri wa kuendelea kununua bidhaa za afya.

  • Waziri Jenista Mhagama Apongeza Mradi wa Ujenzi wa Ghala la Kisasa la MSD-Dodoma

    Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama February 6, 2025 ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma, na kupongeza hatua za maendeleo ya mradi huo wa kimkakati ambao umefikia. asilimia 85%.

  • Wizara ya Afya Somalia, Yaja Kujifunza MSD na Kubadilishana Uzoefu

    Wizara ya Afya nchini Somalia imeichagua  Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kushirikiana kwenye masuala mbalimbali yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya kwa  kubadilishana uzoefu katika maeneo ya mifumo, ununuzi, usambazaji na udhibiti ubora.

  • Bidhaa za Mama na Mtoto

    Hadi kufikia mwaka 2025 MSD tayari imekamilisha ununuzi na usambazaji wa vifaa tiba vya kupambana na vifo vya uzazi pingamizi CEmONC kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. MSD imeweza kufanya ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya Tzs. 100,182,390,897.40 kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya 414. Katika vifaa tiba hivi asilimia themanini (80) imejikita katika vifaa vya upasuaji kama taa za upasuaji, mashine za usingizi, vitanda vya upasuaji ambavyo vimeenda okoa Maisha ya wamama na Watoto nchini Tanzania.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.