Skip to main content
  • Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Atangaza Neema Sekta ya Afya Nchini

    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kuwezesha upatikanaji wa wataalam, dawa, vitendanishi na vifaa tiba.

    Mheshimiwa Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Oktoba 26, 2022 baada ya kushuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Ushirikiano baina ya Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) na Serikali ya Jimbo la Chungcheongbuck nchini Korea kusini.

  • Tanzania Yapokea Msaada Kutoka Benki ya TDB

    DAR ES SALAAM: 

    Serikali ya Tanzania, imepokea msaada wa shilingi milioni 230 kutoka Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB) kwa ajili ya kununulia vifaa vya kujikinga na kupambana na ugonjwa wa Uviko-19.

    Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Uongozi wa benki hiyo, Mkurugenzi wa Uhusiano na Uwekezaji Bi. Mary Kamari, amesema benki yake imetoa msaada huo ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika miradi mbalimbali kimkakati ili kuwaletea Watanzania maendeleo.

  • Katibu Mtendaji SADC Atembelea MSD

    DAR ES SALAAM:

    Katibu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Mhe. Elias Mpedi Magosipamoja na ujumbe wake, wametembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD), yaliyokoKeko jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujionea jinsi taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu yake sambamba na kupokea mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa manunuzi ya pamoja (SPPS) kwaajili ya nchi wanachana.

  • Mkurugenzi Mkuu MSD, Abainisha Mafanikio ya MSD Chini ya Awamu ya Sita

    DODOMA:

    Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bw. Mavere Tukai leo tarehe 17/10/2022amekutana na waandishi wa habari Mkoani Dodoma na kutoamrejesho juu ya mafanikio ya Bohari ya Dawa (MSD) chini yaserikali ya awamu ya sita, inayoongozwaMhe. Samia Suluhu Hassan.

    Bw. Mavere amesema katika mwaka wa fedha 2022/23,MSD imee ndelea kufanya maboresho ya kiutendaji kamailivyoelekezwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku mabadiliko hayoyakilenga kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afyapamoja na utawala bora.

  • Wazalishaji Bidhaa za Afya Kutoka Jamhuri ya Ucheki, Waitembelea MSD

    Wajumbe wa chama cha viwanda vya kuzalisha bidhaa za afya kutoka Jamhuri ya Ucheki (Czech) ambao wako ziarani nchini Tanzania wametembelea Bohari ya Dawa (MSD) na kuelezea maeneo mbalimbali wanayoweza kushirikiana na Tanzania hasa upande wa bidhaa afya.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.