Skip to main content
  • Mtendaji Mkuu Global - Fund, Atembelea MSD

    Dar es Salaam.

    Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Dunia (Global fund) Bw. Peter Sands, amefanya ziara Bohari ya Dawa (MSD) na kujionea namna MSD inavyotekeleza majukumu yake.

    Kupitia ziara hiyo, Mtendaji Mkuu huyo, amepata wasaa wa kutembelea maghala ya kuhifadhia bidhaa za afya, yanayomilikiwa na MSD, yaliyoko Keko, jijini Dar es Salaam.

    Bwana Sands ameahidi kuwa mfuko huo utaendelea  kuiwezesha MSD kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya, hasa za miradi Msonge, huku akiipongeza MSD kwa kufanikisha usambazaji wa vyandarua nchini.

  • Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Atoa Rai kwa Watumishi wa Afya

    Singida.

    Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatma Mganga, ametoa rai kwa MSD na wataalamu wengine wa afya wakiwemo Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaboresha huduma kwenye maeneo yao, ikiwemo upatikanaji wa bidhaa za afya, ili kuwahudumia wananchi kwa utimilifu.

    Dkt. Mganga ametoa rai hiyo leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD na Wadau wake, kilichofanyika Mkoani Singida.

  • MSD Yapongezwa Kuanzisha Mikutano na Wadau Wake

    Dodoma.

    Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Ally Senga Gugu, ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dodoma kwa kukutana na wadau wake na kujadili masuala mbalimbali yahusuyo mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, yanayogusa pande zote mbili kwa lengo la kuboresha huduma na kuleta tija kwa wananchi. 

  • Mhe. Queen Sendiga Aipongeza MSD

    Rukwa.

    Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga amefurahishwa na huduma za MSD Mkoani humo na kusema kwamba hivi sasa huduma za afya hasa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika kwa kiasi kikubwa.

    Mhe. Sendiga ameongeza kuwa huduma na uhusiano wa MSD na Uongozi wa Mkoa wa Rukwa umeimarika na kwamba kero mbalimbali zilizokuwepo hapo awali, mathalani za upungufu wa bidhaa za afya sasa zimetatuliwa kwa kiasi kikubwa.

  • Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Atoa Rai - Matumizi ya Vyandarua

    Kongwa.

    Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius M. Emmanuel amewataka wakazi na wazazi wote wilayani humo kutumia vyema na kwa lengo lililokusudiwa vyandarua vya msaada wanavyopatiwa serikali, ili adhima ya serikali ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iweze kutimia.

    Mhe. Remidius ametoa rai hiyo hii leo wakati akizindua rasmi zoezi la usambazaji wa vyandarua mashuleni wilayani humo, linalofanya na Bohari ya Dawa (MSD).

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.