Skip to main content
New MSD Employees Receive Systems Training

Watumishi wapya MSD Wapatiwa Mafunzo ya Mifumo

Watumishi wapya MSD wamepatiwa mafunzo ya namna ya kutumia mifumo ya kiutendaji ya MSD ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao.

Mafunzo hayo yanayofanyika MSD Keko jijini Dar es Salaam ni ya siku kumi na yanahusisha mifumo yote ambayo watumishi hao wataitumia katika kutoa huduma kwa wateja na wadau mbalimbali wa MSD. 

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkufunzi wa mafunzo hayo Emmanuel Mnzava ambaye ni Afisa TEHAMA Mkuu wa MSD amesema kila mtumishi anaeajiriwa au kuhamishiwa MSD anapaswa kupata mafunzo ya namna ya kutumia mifumo mbalimbali ya kiutendaji ambayo itamuwezesha katika utoaji wa huduma kwa ufasa. 

Mnzava ameongeza kuwa mifumo ndio nyenzo kubwa inayowezesha MSD kuendesha shughuli zake za kila siku ikiwemo kuhudumia wateja na wadau wake, pia kuhifadhi kumbukumbu za taasisi.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.