Skip to main content

Wateja wa MSD Kanda ya Tanga Wapongeza Maboresho ya Huduma za MSD

Wateja wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Tanga wameipongeza MSD kwa maboresho makubwa inayoendelea kuyafanya ya usambazaji wa bidhaa za afya kwa wakati.

Pongezi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD ambaye pia ni Mlezi wa MSD  kanda hiyo, Dkt. Rukia Mwifunyi anayoifanya mkoani humo, kuzungumza na wateja wanaowahudumia ili kupata maoni yao juu ya huduma za MSD na kupokea changamoto zao ili ziweze kufanyiwa kazi.

Ziara hiyo inafanyika ikiwa ni moja ya matukio ya kuadhimisha miaka 30 ya utendaji wa MSD tangu 1994,ambapo kabla ya hapo ilikuwa ikiitwa Central Medical Store (CMS)

Mfamasia wa Hospitali ya Mkoa wa Tanga (Bombo), Kibwana Mgude alipongeza MSD kwa kuwafikishia bidhaa za afya kwa wakati na kueleza kuwa sasa upatikanaji wa bidhaa za afya umeboreshwa kwa kiwango cha juu.

“ Sasa hivi tunapokea dawa na vifaa tiba kwa wakati tunakila sababu ya kupongeza maboresho haya ya MSD,” alisema Mgude.

Kwa upande wake Magdalena Chambo ambaye ni Muuguzi wa Kituo cha Afya cha Nkumba alisema utaratibu unaofanywa na MSD wa kuwapelekea bidhaa za afya hadi vituoni mara sita (6) kwa mwaka ni mzuri.

Dkt. Mwifunyi akizungumza wakati wa ziara hiyo alipongeza MSD kwa kazi kubwa wanayoifanya ambapo alitumia nafasi hiyo kuomba kudumisha ushirikiano baina yao na wateja wao wanaowahudumia.Aliwasisitiza wateja hao wa MSD kutoa mapendekezo yao ambayo wataona yana tija kwa ajili ya kuboresha shughuli zinazofanywa na MSD.

“ Utoaji wa huduma bora za usambaji wa vifaa tiba na dawa ni jambo jema kwani jamii na taifa wanatutegemea,” alisema Dkt. Mwifunyi.

Katika ziara hiyo Dkt. Mwifunyi aliongozana na baadhi ya maafisa wa MSD kutoka Kanda ya Tanga na Makao Makuu wakiongozwa na Meneja Huduma za Sheria MSD, Elisamehe Macha, MenejaMawasiliano naUhusiano wa MSD Bi. Etty Kusiluka na Meneja Huduma kwa Wateja Dkt. Pamella Sawa.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.