Skip to main content

Wizara ya Afya Somalia, Yaja Kujifunza MSD na Kubadilishana Uzoefu

Wizara ya Afya nchini Somalia imeichagua  Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kushirikiana kwenye masuala mbalimbali yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya kwa  kubadilishana uzoefu katika maeneo ya mifumo, ununuzi, usambazaji na udhibiti ubora.

Hayo yamebainishwa na watendaji wa Wizara ya Afya kutoka nchini Somalia waliotembelea Bohari ya Dawa (MSD), ambapo mwakilishi wa ugeni huo Mohamed Abdulukadiri Hersi  ameeleza kuwa  hatua mbalimbali zilizofanywa na Serikali ya  Tanzania kupitia Bohari ya Dawa katika mifumo inayotumika katika mnyororo mzima wa ugavi inayotumia tekinolojia ndio umewavutia zaidi kuja kujifunza kwa kujionea namna inavyofanya kazi na kuoana na mifumo mingine ya serikali.

Hersi  ameongeza kuwa, Somalia ipo kwenye mpango wa kujenga upya mfumo wake wa ugavi wa bidhaa za afya, ikiwa ni pamoja na kuboresha utaratibu wa kufikisha bidhaa za afya kwa wananchi, hivyo kati ya nchi walizozichagua kuwa mfano ni Tanzania, ambapo kupitia MSD amesema wamemejifunza mengi ambayo watakwenda kuyatekeleza watakaporudi. 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai, ameeleza kuwa wageni hawa wamekuja Tanzania kwa muda muafaka ambapo MSD imefanya mageuzi makubwa ya kiutendaji ikiwemo kujiendesha kibiashara, na kufanya maboresho mbalimbali katika mnyororo mzima wa ugavi wa bidhaa za afya, hivyo watajifunza mengi.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.