Skip to main content
MSD Peer Educators Educated

Waelimisha Rika MSD Wanolewa

Dar es salaam

Waelimisha rika (Pear Educators) ambao ni Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wanapatiwa mafunzo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa yasiyoambukiza. 

Mafunzo hayo ya siku tatu yanahusisha waelimika rika kutoka Kanda na Idara zote za MSD, ambao watakuwa waelimishaji watumishi wengine.

Sera ya MSD ya kukinga watumishi dhidi ya UKIMWI na magonjwa yasiyoaambukiza inaeleza kuwa kila Kanda na Idara ya MSD inatakiwa kuwa na mueleimisha rika ili aweze kuwasaidia watumishi wengine namna ya kujikinga dhidi ya UKIMWI na magonjwa yasiyoambukiza. 

Mkufunzi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Kweka amesema Elimu ya UKIMWI mahali pa kazi inawawezesha watumishi kuzingatia mihimili muhimu kuwa na uhakika wa elimu na habari za magonjwa tajwa, mafunzo,ufahamu wa kupima kwa hiari, matunzo na kusaidia waathirika.

Aidha watumishi watakuwa chachu katika kampeni ya kujikinga na kudhibiti magonjwa hayo.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.