Skip to main content
Misonge MSD Project Manager, Elias Katani Briefing USAID and PEPFAR Leaders During Their Visit to MSD Offices in Iringa Region

Uongozi wa Juu USAID na PEPFAR Watembelea MSD Kanda ya Iringa

Mkurugenzi Mkazi wa USAID Tanzania Craing Hart na Mratibu Mkuu wa PEPFAR Tanzania Jessica Greene wametembelea MSD Kanda ya Iringa kuangalia namna MSD inavyotekeleza Majukumu yake, hasa ununuzi, utunzaji, na usambazaji wa bidhaa za afya zinazofadhiliwa na Mifuko hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ziara hiyo, Bw. Hart na Bi. Greene wameipongeza MSD kwa weledi wake katika usimamizi na usambazaji wa bidhaa za miradi misonge hadi kwa walengwa ambao ni wananchi.

Viongozi hao pia wamepongeza uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na Serikali ya Marekani kupitia miradi ya USAID na PEPFAR, huku wakisisitiza kwamba, ushirikiano kupitia miradi hiyo umesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha na kuimarisha afya za Wananchi.

Katika hatua nyingine wameipongeza MSD kwa kujidhatiti katika adhma yake ya kujiendesha kibiashara, kwani ni hatua nzuri kuelekea uchumi imara na huduma za uhakika.

Aidha, wameahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania, pamoja na wadau mbalimbali ikiwemo MSD, katika nyanja mbalimbali kwa kadri ya mahitaji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Bi. Rosemary Slaa ameishukuru serikali ya Marekani kupitia miradi yake kwa kuendelea kuisaidia Tanzania.

Ameongeza kuwa MSD inasambaza bidhaa nyingi zilizoko chini ya wafadhili hao, mathalani bidhaa za UKIMWI, Malaria, pamoja na bidhaa za mama na mtoto.

Rosemary pia amedokeza kwamba MSD imekua mnufaika mkubwa kupitia ujenzi wa maghala, usimikaji mifumo, na ununuzi wa magari ya usambazaji kupitia ufadhali wa wadau hao.

Hata hivyo, ameeleza kwamba bado MSD inakabiliwa na ufinyu wa maghala ya kuhifadhia bidhaa za afya, kutokana na ongezeko la watu, vituo vya afya, zahanati na hospitali nchini, hivyo kuwaomba wadau hao kuendelea kuisaidia MSD, Ili iweze kusimama imara katika mnyororo wa ugavi.

Ziara hiyo imekuja ikiwa ni maadhimisho ya miaka 20 toka kuanzishwa kwa Mfuko wa PEPFAR.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.