Skip to main content

Ujumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Watembelea Kanda ya Kilimanjaro

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini MSD Dkt. Ritah Mutagonda, ambaye pia ni mlezi wa MSD Kanda ya Kilimanjaro ameipongeza Kanda ya MSD Kilimanjaro kwa kuvuka lengo la mauzo kwa kufikia 115% katika kipindi cha nusu mwaka wa fedha 2024/2025.

Mjumbe huyo wa Bodi ya Wadhamini ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake kwa wateja wanaohudumiwa na Kanda ya Kilimanjaro, kama moja ya shughuli za kuadhimisha miaka 30 ya utendaji wa MSD.

Dkt. Mutagonda pia amemwelekeza Meneja wa Kanda kuhakikisha waaimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya hususani  zile za huduma maalum, ili kuboresha utendaji katika vituo vya kutolea huduma za afya. 

Akizungumza na watumishi wa Kanda ya Kilimanjaro, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa MSD, Jafari Makoka ambaye amefuatana na Mjumbe wa Bodi katika ziara hiyo, amewasisitiza watumishi wa MSD kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi, umakini, uaminifu na kufuata sheria na utaratibu.

Ujumbe wa MSD ulitembelea hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi na kuzungumza na uongozi wa hospitali hiyo, ambapo pamoja na mambo mengine walieleza kuridhishwa na huduma za MSD.

Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Edna Munisi amewaeleza MSD kuwa wapo katika hatua za mwisho za kukamilisha jengo la huduma ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo, na tayari imeshapokea baadhi ya mashine kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Ziara hiyo imeendelea katika kituo cha afya kilichoongezwa hadhi cha Uru, wilayani Moshi na Zahanati ya Rau iliyopo Manispaa ya Moshi.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.