Skip to main content

Ujumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Watembelea Hospitali za Mkoa wa Simiyu

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Bw. Ally Seleman, akiambatana na Kaimu Meneja Mipango,Tathimini na Ufuatiliaji leo tarehe 20/11/24 wametembelea Kanda ya MSD Mwanza na kujionea jinsi Kanda hiyo inavyotekeleza majukumu yake,  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa MSD.

Kupitia ziara hiyo Bw. Selemani amepokea taarifa ya utendaji wa Kanda hiyo, sambamba na mipango mbalimbali ambayo Kanda hiyo imejiwekea Ili kuhakikisha inaboresha huduma zake.

Bw. Selemani ameipongeza Kanda hiyo kwa jinsi inavyotekeleza majukumu yake, licha ya eneo kubwa inalohudumia, huku akiahidi kutafutia ufumbuzi baadhi ya changamoto zinazoikabili Kanda hiyo, ili kuongeza ufanisi zaidi.

Katika hatua nyingine ujumbe huo wa MSD, ukiongozwa na Bw. Selemani umetembelea hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu, sambamba na Hospitali ya Wilaya ya Bariadi  kutathimini hali ya upatikanaji wa huduma za MSD Mkoani hapo.

Akimzungumza wakati wa ziara hiyo Mganga Mfawidhi wa hospitali Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, Dkt. Athanas Ngambakubi ameipongeza MSD kwa kuboresha huduma zake, ukilinganisha na kipindi cha nyuma kwani hivi sasa upatikanaji wa Dawa na Vifaa tiba umeimairika kwa zaidi ya asilimia 70 hospitalini hapo.

Aidha amebainisha kwamba Ubora wa bidhaa za MSD umekuwa wa uhakika, huku gharama ya bidhaa hizo ikiwa ni rafiki zaidi kuliko washitiri wengine.

Naye Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Bariadi Dkt. Maghembe Kuligwa amebaisha upatikanaji wa bidhaa za afya hospitalini hapo kuwa zaidi ya asilimia 90, huku akipongeza MSD kwa kuboresha huduma zake, mathalani usambazaji wa Dawa sambamba na upatikanaji wa Vifaa tiba, ulikilinganisha miaka ya nyuma.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.