Skip to main content
Tanzania Receives Assistance From TDB Bank

Tanzania Yapokea Msaada Kutoka Benki ya TDB

DAR ES SALAAM: 

Serikali ya Tanzania, imepokea msaada wa shilingi milioni 230 kutoka Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB) kwa ajili ya kununulia vifaa vya kujikinga na kupambana na ugonjwa wa Uviko-19.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Uongozi wa benki hiyo, Mkurugenzi wa Uhusiano na Uwekezaji Bi. Mary Kamari, amesema benki yake imetoa msaada huo ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika miradi mbalimbali kimkakati ili kuwaletea Watanzania maendeleo.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya serikali, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), ameipongeza benki hiyo kwa mchango wake kwa sekta ya afya, huku akiisihi kuendelea kushirikiana na serikali kwenye nyanja mbalimbali za maendeleo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe amesema Wizara imepokea msaada huo kwa unyenyekevu mkubwa kwani utasaidia katika mapambano ya milipuko ya magonjwa yanayoshabihiana na Uviko-19 mathalani mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, uliozikumba nchi jirani.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.