Skip to main content

Somalia Kushirikiana na MSD, Ununuzi wa Bidhaa za Afya

Rais wa Somalia Mheshimiwa Hassan Sheikh Mohamud amesema nchi yake imeamua kushirikiana kwa karibu na Bohari ya Dawa ya Tanzania katika ununuzi wa bidhaa za afya na kubadilishana uzoefu wa namna mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya unavyofanya kazi.

Rais Mahamud ambaye yuko ziarani nchini Tanzania, ameyasema hayo alipoitembelea MSD, na kuongeza kuwa kutokana na uzoefu wa MSD, wana uhakika kuwa ubora wa bidhaa za afya utakuwa wa uhakika.

Naye Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu ameeleza kuwa kwa kuwa sasa Somalia ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanzania kupitia MSD itaweza kununua bidhaa za afya kwa pamoja ili kupata bidhaa hizo kwa bei nafuu.

Ameongeza kuwa, Marais wa nchi hizo mbili, yaani Tanzania na Somalia wamewapa maelekezo Mawaziri wa Afya nchi zao kukaa pamoja na kuangalia namna ya kushirikiana katika masuala ya upatikanaji wa bidhaa za afya kwa urahisi, kuzingatia ubora na kwa bei nafuu.

Kiongozi huyo wa Somalia na ujumbe wake alizungumza na viongozi wa Wizara ya Afya, Menejimenti ya MSD na kutembelea ghala la kuhifadhia dawa la makao makuu MSD.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.