Skip to main content
Some Citizens of Ifakara Town Council Ward, Kilombero District Participating in Unloading Health Products From an MSD Truck, Which Brought Health Products to the District

Serikali Yakabidhi Vifaa Tiba vya Milioni 900 Halmashauri ya Ifakara

#MOROGORO

SERIKALI kupitia Bohari ya Dawa (MSD), imekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya sh milioni 900 kwa Halmashauri ya Ifakara mji.

Akizungumza jana Mkoani humo, Mbunge wa Kilombero Mhe.Abubakar Asenga, alisema ujio wa vifaa hivyo, utasaidia kuboresha huduma za afya hivyo wanaishukuru serikali kwa hatua kubwa ya maboresho katika sekta hiyo.

Alieleza kuwa, jimbo hilo lilikuwa na kero saba muhmu na kubwa ambazo hazijawahi kutatuliwa tangu kupata Uhuru lakini Rais Dk. Samia amezitatua ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara, maji, ukarabati kituo cha umeme Kidatu,ujenzi wa shule za kata, vituo vya afya, zahanati na hospitali.

Naye Mkuu wa wilaya ya Kilombero Dunstan Kyobya amesema ujio wa vifaa tiba hivyo ni neema kwa halmashauri hiyo.

Alisema, maboresho hayo makubwa yanayofanywa na Rais Dk.Samia ni lazima kuungwa mkono na watendaji hivyo anatoa siku 15 kuhakikisha MSD inafunga vifaa hivyo na wananchi wanaanza kupata huduma.

“ Niwaombe MSD ilete wataalamu wao kwa ajili ya kufunga vifaa hivi, haiwezekani Rais wetu afanye mambo makubwa kama haya watendaji tumuangushe, ni muhimu kuhakikisha tunasimamia na wananchi wanaanza kupata huduma kwa wakati,”alisema.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa MSD ambaye ni Mfamasia na Afisa Huduma kwa Wateja Kanda ya Dar es Salaam Diana Kimario, alisema kanda hiyo ina hudumia mikoa mitatu ambayo ni Dar es salaam, Pwani, Morogoro ambapo Ifakara ni mnufaika.

“Ujio wa vifaa hivyo vyenye thamani ya sh. milioni 900 ni muendelezo wa mabadiliko makubwa katika maboresho sekta ya afya, sisi watumishi ndani ya MSD tunajivunia namna serikali yetu chini ya Rais Dk. Samia, Waziri wetu wa afya Mhe. Ummy Mwalimu na Mkurugenzi wa MSD Mavere Tukai wanavyohakikisha tunafanya kazi kwa weledi.

Aliongeza kuwa kama MSD, wamejipanga kupitia maboresho ya ndani, ikiwemo mikataba, ili kuhakikisha Dawa na Vifaa tiba vinapatikana kwa wakati, na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya nchini.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.