Skip to main content
The Egyptian Government Provides Medical Equipment Assistance to Tanzania

Serikali ya Misri Yatoa Msaada wa Vifaa vya Matibabu kwa Tanzania

Ubalozi wa Misri nchini Tanzania leo Septemba 8, 2022 umetoa msaada wa vifaa tiba kwa Serikali ya Tanzania ili kuboresha huduma za afya nchini.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya dola za kimarekani elfu 27 (USD 27,000) ambazo ni sawa na takriban shilingi milioni 62.9 za kitanzania, vimekabidhiwa rasmi kwa serikali ya Tanzania.

Akikabidhi msaada huo Balozi wa Misri nchini Mhe. Mohamed Gaber Abuwafa amesema kuwa serikali ya Misri itaendelea na juhudi za kuiunga mkono serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za afya.

“Serikali ya Misri kupitia shirika lake la EAPD imetoa msaada huu ili kuboresha huduma za afya, ikumbukwe kuwa huu sio msaada wa kwanza na hautakuwa wa mwisho, kwani nchi zetu zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu katika nyanja mbalimbali, hivyo pamoja na msaada huu, tunatarajia kuanzisha ushirikiano katika siku zijazo katika kubadilishana utaalamu na wataalamu kupitia sekta ya afya”. Alisisitiza Balozi Mhe. Abuwafa

Mhe. Abuwafa ameongeza kuwa, serikali ya Misri inaangalia uwezekano wa kuwekeza nchini humo katika sekta ya dawa na vifaa vya matibabu, ili kuendeleza uhusiano wa muda mrefu kati ya pande hizo mbili.

“Serikali ya Misri itaendelea kuunga mkono sekta mbalimbali nchini ikiwemo uanzishwaji wa viwanda vya kutengeneza dawa ili kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan katika kuboresha na kusogeza huduma za afya karibu na jamii kwa bei nafuu,” alisema Balozi Abuwafa.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi, aliishukuru Serikali ya Misri kupitia ubalozi wake nchini, kwa kuipatia Tanzania msaada huo, na kusisitiza kuwa utakuwa chachu ya kuboresha afya za wananchi wake.

“Kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, tunaipongeza na kuishukuru Serikali ya Misri kwa kutupatia msaada huu ili kuboresha afya za Watanzania na ushirikiano uliopo kati ya mataifa yetu, tunatarajia huu hautakuwa msaada wa mwisho, bali ni mwendelezo wa ushirikiano zaidi kati ya mataifa yetu. Alisema Msasi

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.