Skip to main content
Acting Director of Supply and Operations of MSD Mr. William Singano, Speaking to Medical Equipment and Bar Specialists in the Country, During the Closing of Training, in Morogoro Region

MSD Yatoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Vifaa Tiba na Maabara Nchini.

Mafunzo ya siku tatu kwa wahandisi wa vifaa tiba na wataalam wa maabara nchini yamehitimishwa leo mkoani Morogoro.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa wakati mmoja katika mikoa mitano kwa wataalam kutoka nchi nzima, yalilenga kutoa mafunzo kwa wataalam wa ufungaji, matumizi na matengenezo ya mashine na vifaa vya maabara vinavyosambazwa na MSD.

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji Bw.William Singano alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wahandisi wa vifaa tiba na wataalamu wa maabara kwani yanawawezesha watumiaji kumudu kuvitumia, kuvitunza na kuvitengeneza.

Mheshimiwa Singano ameitaka Serikali kuboresha huduma za afya kwa kuwezesha mashine na vifaa vya kisasa kote nchini. Mafunzo hayo yametolewa katika mikoa ya Tabora, Morogoro, Mbeya, Kilimanjaro na Mwanza ambapo wataalam kutoka mikoa mingine yote walijumuika kupata mafunzo hayo.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.