Skip to main content

MSD YAKABIDHI JENERETA LA KVA 75 KWA HOSPITALI YA WILAYA YA KITETO

Hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto mkoani Manyara imeondokana na changamoto ya kukatiza baadhi ya huduma za matibabu kama upasuaji na pindi umeme unapokatika baada ya Bohari kuu ya dawa MSD kukabidhi jenereta lenye thamani ya shilingi milioni 65 itakayotumika kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano mjini Kibaya wilayani Kiteto, meneja wa MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema jenereta hilo lenye uwezo wa KVA 75 ni sehemu ya mahitaji ya vifaa vya afya vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 699 vilivyoagizwa na hospitali hiyo kwa bohari kuu ya dawa MSD katika mwaka wa fedha 2023/2024. 

Amesema tayari MSD imeshakabidhi vifaa vingine vilivyoagizwa katika hospitali hiyo vyenye thamani ya shilingi milioni 683 sawa na asilimia 98 ya vifaa vilivyoagizwa na halmashauri hiyo kupitia MSD na ameahidi wakati wowote kuanzia sasa kukamilisha sehemu iliyobaki ambayo ni mfumo wa kuhifadhi miili (mortuary cabinet).  Mganga mkuu wa wilaya ya Kiteto Dkt Vicent Gyunda ameshukuru bohari kuu ya dawa kanda ya Dodoma kukabidhi jenereta hilo kwa wakati ambayo sasa   itawezesha uhakika wa huduma za upasuaji wa wagonjwa, kuwapa joto watoto njiti pamoja na huduma ya kuhifadhi maiti. 

Akizungumza katika hafla hiyo mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga ameagiza uongozi wa hospitali ya Halmashauri hiyo kutenga bajeti ya mafuta ya jenereta hilo ili litumike wakati wowote pindi umeme unapokatika. Wilaya ya Kiteto ni miongoni mwa maeneo ambayo huduma ya umeme hukatika kila mara kutokana na uchakavu wa miundombinu hali ambayo imekiwa ikitatiza utoaji wa huduma za kitabibu zinazohitaji uwepo wa umeme katika hospitali ya Halmashauri ya wilaya hiyo mjini Kibaya.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.