Skip to main content
MSD Improves Hemodialysis Services - Tumbi Hospital

MSD Yaboresha Huduma za Kusafisha Damu- Hospitali ya Tumbi

PWANI

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani - Tumbi imeanza kutoa huduma mpya ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo. Huduma hii imeanza kutolewa baada ya Bohari ya dawa (MSD) kukamilisha usimikaji wa mashine za kisasa 10 za kusafisha damu, baada ya hospitali ya rufaa ya Tumbi kuboresha miundombinu ya kuwezesha huduma hiyo kupatikana.

Hatua hiyo ni muendelezo wa maboresho ya huduma za afya nchini yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Afya.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Amani Malima amesema mpaka sasa tayari huduma imeshatolewa kwa wagonjwa watatu na huduma hiyo imefanikiwa kwa asilimia 100.

Kwa upande wake Fundi Sanifu vifaa tiba wa MSD Ikunda Harrison amesema mbali na kufunga mashine hizi MSD ilitoa mafunzo kwa watoa huduma wa hospitali hiyo, ambapo kwa sasa jukumu kubwa la MSD ni kuhakikisha vitendanishi vya mashine hizo vinaendelea kuwepo wakati wote ili kuepuka kukwamisha huduma

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.