Skip to main content
Kongwa District Commissioner Gives Opinion - Use of Nets

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Atoa Rai - Matumizi ya Vyandarua

Kongwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius M. Emmanuel amewataka wakazi na wazazi wote wilayani humo kutumia vyema na kwa lengo lililokusudiwa vyandarua vya msaada wanavyopatiwa serikali, ili adhima ya serikali ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iweze kutimia.

Mhe. Remidius ametoa rai hiyo hii leo wakati akizindua rasmi zoezi la usambazaji wa vyandarua mashuleni wilayani humo, linalofanya na Bohari ya Dawa (MSD).

"lengo serikali kuwagawia vyandarua ni kuwakinga watoto wetu dhidi ya ugonjwa hatari wa Malaria, hivyo naomba vitumike kama ilivyokusudiwa na kwa matumizi ambayo ni kinyume na matakwa ya lengo la serikali kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria. Alisema Mhe. Remidius.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma, Bw. John Sipendi amesema MSD imejipanga vizuri kusambaza vyandarua kwenye shule zote zilizoainishwa na kwa muda uliopangwa.

" Sisi kama MSD tumejipanga kuhakikisha tunatekeleza zoezi hili la usambazaji kwa ufanisi na kwa wakati, hivyo niwatoe hof kwani hakuna shule itakosa vyandarua.

Bw. Sipendi ameongeza kuwa tayari magari ya usambazaji yako wilayani humo, na jumla ya vyandarua 87,038 vitasambazwa kwenye shule za msingi 123.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.