Skip to main content
Njombe Regional Commissioner Visits MSD-Idofi Factory

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Atembelea Kiwanda cha MSD-Idofi

NJOMBE

Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Njombe imetembelea kiwanda cha Bohari ya Dawa (MSD) cha kuzalisha mipira ya mikono kilichopo Idofi, Makambako ambacho ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 70.

Mhe.Mtaka amesema kiwanda hicho ni muhimu kwa sekta ya afya kwani kitapunguza matumizi ya fedha za kigeni kununua bidhaa hiyo nje ya nchi na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa mipira ya mikono nchini.

Mtaka aliiagiza MSD ikamilishe kiwanda hicho ili uzalishaji uanze ili wananchi wanufaike na mradi huo na kutafuta masoko nchi za SADC.

Mwenyekiti wa bodi ya Wadhamini ya MSD Rosemary Silaa amesema kiwanda hicho kitatoa ajira 200 huku Mkurugenzi Mkuu MSD Mavere Tukai akieleza kuwa uzalishaji wa mipira ya mikono kiwandani hapo unatarajiwa kuanza mwezi Julai mwaka huu.

Uzalishaji wa kiwanda hicho utaiwezesha MSD kukidhi mahitaji yake kwa asilimia 83.4 ya mahitaji ya mipira ya mikono nchini.

Kwa upande wake Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi amesema serikali kupitia Wizara ya Afya inaunga mkono uanzishwaji wa viwanda vya bidhaa za afya, na watahakikisha kiwanda hicho kinaanza uzalishaji.

Kiwanda hicho kitaokoa matumizi ya fedha za kigeni Bilioni 24 kwa mwaka ambazo zingenunua bidhaa hiyo nje ya nchi.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.