Skip to main content
Mavere from MSD with Maswi from PPRA

Mkurugenzi Mkuu MSD, Afanya Mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA (CEO)

Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw.Mavere Ali Tukai amefanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Bw.Eliakim C.Maswi kuhusu namna bora ya kuboresha ununuzi wa bidhaa za afya kufuatia changamoto kadhaa zinazoikabili Bohari ya Dawa katika eneo hilo.

Mavere amemueleza Mtendaji Mkuu huyo mtazamo wake kuhusu manunuzi katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria, taratibu, miongozo na mfumo wa TANEPS.

Kupitia mkutano huo, Mavere amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili Bohari ya Dawa katika masuala ya manunuzi, na namna bora ya kuzitatua, ili kuboresha upatikanaji wa Dawa na Vifaa Tiba nchini.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA amempongeza Bw.Mavere kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo huku akiahidi kuzifanyia kazi haraka changamoto mbalimbali za manunuzi zinazoikabili MSD.

Ununuzi wa Umma

Aidha, alisisitiza kuwa taasisi za umma zina mahitaji tofauti, hivyo kuahidi kuangazia na kutatua changamoto zilizoainishwa ili kuboresha manunuzi ya umma.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.