Skip to main content
MSD Drivers Build Capacity

Madereva wa MSD Wajengewa Uwezo

MOROGORO.

Watumishi wa MSD wa kada ya Udereva, wameendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo mbalimbali, yanayoandaliwa na taasisi mathalani udereva wa kujihami, alama za barabarani, ukaguzi wa magari, sheria za usalama barabarani, upakiaji wa mizigo na namna bora ya kuendesha magari makubwa yanayovuta tella (truck and trailers) ili kuongeza tija katika kazi zao na taasisi kwa ujumla.

Mafunzo hayo ya siku 10 yamehusisha nadharia na vitendo na yametolewa na wataalamu kutoka Chuo cha Ufundi Veta, kilichoko Mkoani Morogoro.

Kwaupande wake Mkufunzi wa Chuo hicho Bw. William Emmanuel Munuo, ambaye amekuwa akiendesha mafunzo hayo ameipongeza MSD kwa kuratibu mafunzo hayo, kwani yamekua na tija kwa wanafunzi wake.

"Teknolojia zinabadilika katika magari, alama za usalama zinaongezeka, barabara zinabadilika, hivi sasa nchini zipo barabara za juu na chini, hivyo ni vyema kuwanoa maderava wetu ili waweze kwenda na wakati, niwapongeze MSD kwa kuliona hilo" Alisema Bw.Mnuo

Akizumgumza kwaniaba ya Maderava wa MSD Bw. Marwa Wangwe, amesema mafunzo hayo yamewaongezea ujuzi, kujiamini na uelewa wa masuala mbalimbali ya muhimu katika uedenshaji wa vyombo vya moto.

Aidha ameiomba Menejimenti ya MSD, kuratibu mafunzo hayo mara kwa mara, ili kuwajengea uwezo na kuongeza tija katika utekelezaji wa shughuli za taasisi.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.