Skip to main content
Singida Regional Administrative Officer, Dr. Ally Fatma Mganga (Standing), Addressing During the MSD Session with Its Stakeholders from Singida Region

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Atoa Rai kwa Watumishi wa Afya

Singida.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatma Mganga, ametoa rai kwa MSD na wataalamu wengine wa afya wakiwemo Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaboresha huduma kwenye maeneo yao, ikiwemo upatikanaji wa bidhaa za afya, ili kuwahudumia wananchi kwa utimilifu.

Dkt. Mganga ametoa rai hiyo leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD na Wadau wake, kilichofanyika Mkoani Singida.

Ameongeza kuwa serikali ya Awamu ya Sita imejenga vituo vingi vipya vya kutolea huduma za afya nchini na kuviongeza hadhi vingine, hivyo kazi kubwa kwa MSD ni kuhakikisha bidhaa za afya hitajika katika vituo hivyo zinapatikana kwa wakati na huduma za afya zinatolewa kwa wananchi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victoria Ludovick, ameipongeza MSD kwa kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya Mkoani humo, ambapo kwa sasa umefikia asilimia 88%.

Hata hivyo, ameisihi MSD kuendelea kuboresha upatikanaji huo ili uwe maradufu, mathalani upatikanaji wa vifaa tiba.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma. Bw. John Sipendi, amewashukuru wadau hao kwa kuitia mualiko huo, huku akihimiza umuhimu wa mijadala ya wazi ili kupata suluhu ya changamoto mbalimbali na hatimae kutoka na maazimio ambayo yatasaidia kuboresha huduma kwa pande zote mbili.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.