Skip to main content

Ujumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Watembelea Kanda ya Mbeya

Mwakilishi wa wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Bohari ya Dawa (MSD), Dr. Alex Magesa, ambaye alifuatana na Mkurugenzi wa Ununuzi Hamis Mpinda wamefanya ziara katika Kanda ya MSD, Mbeya, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa MSD.

Katika ziara hiyo  viongozi  hao walitembelea wateja wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya na kuzungumza nao kuweza kujua namna wanavyozipokea huduma za MSD na kujadili kwa pamoja namna ya kuboresha huduma hizo.

Akizungumza baada ya ziara hiyo mjumbe huyo wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Dr. Magesa amesema kuwa wameweza kutembelea ghala la kanda ya Mkoa wa Mbeya na kujionea jinsi shughuli za ugavi wa bidhaa za afya zinavyofanyika.

Dr. Magesa ameeleza kuwa,  amefurahishwa na ari ya watumishi wa MSD Kanda ya Mbeya na utendaji wao ambapo umeonyesha kiwango cha juu cha juhudi na weledi.

Naye Mkurugenzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji ameishukuru MSD kwa huduma bora wanazotoa na ushirikiano wa karibu ambao umesaidia hospitali hiyo kupata bidhaa za afya kwa wakati zikiwa na ubora unaostahili.

Naye Kaimu Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya, Petro Mdegela, amesema ziara hiyo pia itahusisha kituo cha afya na zahanati ili kuweza kupata mrejesho wa huduma zinazotolewa na MSD katika ngazi zote za vituo vya kutolea huduma za afya.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.