Skip to main content
MSD Monitors Drug Quality in Clinics at Muheza Hospital

MSD Yafuatilia Ubora wa Dawa-Vituoni

Bohari ya dawa (MSD) kupitia Kitengo chake cha Udhibiti Ubora imeendelea na zoezi la ufuatiliaji wa ubora wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ambavyo vimeshasambazwa kwa wateja ili kuhakikisha bidhaa hizo za afya hasa dawa, zinaendelea kuwa na ubora unaotakiwa.

Zoezi hili ni muongozo uliotolewa na Shirika la Afya duniani (WHO) pamoja na ushauri wa Mamlaka ya Dawa na vifaa tiba (TMDA) kuitaka MSD kama msambazaji wa bidhaa za afya nchini kufuatilia ubora wa bidhaa ambazo tayari zipo kwa wateja na kujionea jinsi zinavyotunzwa, ili kulinda afya za watumiaji kwani kumekuwepo na changamoto nyingi kwenye mnyororo wa ugavi wa dawa, zinazoweza kuathiri ubora wa awali wa dawa na vifaa tiba, ikiwemo namna ya usafirishaji, utunzaji na hali ya hewa kwenye maeneo yao.

Katika mwaka wa Fedha 2022/2023 tayari zoezi hili limeshafanyika katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Kilimanjaro na Tanga kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati, huku zoezi hilo likitarajiwa kuendelea kwenye mikoa mingine.

Zoezi hili hutekelezwa kila mwaka ili kulinda afya za watumiaji ikiwa ni pamoja na kushauri juu ya mapungufu yatakayoonekana katika vituo vya kutolea huduma za afya, ili kuepusha athari za ubora wa bidhaa hizo.

Zoezi hili huangazia namna ya usafirishaji, utunzaji na hali ya hewa kwenye maeneo ambapo bidhaa hizo huhifadhiwa katika vituo hivyo.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.