Aller au contenu principal

Katibu Tawala Dar es Salaam apongeza MSD kwa utekelezaji bora


Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Abdul Mhinte, ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dar es Salaam kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake, huku akitoa wito kwa watendaji wa sekta ya afya mkoani humo kuhakikisha wanadhibiti na kusimamia vyema ukusanyaji wa mapato kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kuwezesha ulipaji wa madeni kwa wakati.

Akizungumza leo, Septemba 17, 2025, jijini Dar es Salaam wakati wa kufungua kikao cha wateja na wadau wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, Mhinte amesema kuwa usimamizi mzuri wa mapato yatokanayo na huduma za afya ni muhimu katika kuhakikisha vituo vinaweza kununua bidhaa muhimu na kusimamia vyema mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuongeza bajeti ya ununuzi wa bidhaa za afya ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Mhinte ameongeza kuwa uwepo wa kikao hicho ni chachu ya kutoa uelewa zaidi kuhusu mifumo ya MSD, kubadilishana uzoefu na kujadili namna bora ya kushirikiana ili kuboresha utoaji wa huduma za afya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD, Victor Sungusia, amesema kuwa serikali imeongeza bajeti ya dawa kutoka Shilingi bilioni 200 hadi bilioni 300 kwa mwaka, ikiwa ni sehemu ya kuboresha huduma za afya nchini.

“Tunaendelea kuboresha utendaji kazi wetu, kuhakikisha huduma inapatikana kwa wakati. Naomba washiriki wa kikao hiki mtoe mrejesho ili tuweze kuboresha zaidi,” amesema Sungusia.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, Betia Kaema, amesema kuwa MSD inajenga mfumo madhubuti wa ununuzi, utunzaji na usambazaji wa bidhaa za afya kwa kutumia mbinu na ushauri wa kitaalamu.

Ameongeza kuwa upatikanaji wa bidhaa za afya umeongezeka kutoka asilimia 54 katika mwaka wa fedha 2023/24 hadi asilimia 74, na wanatarajia kufikia asilimia 90 katika mwaka wa fedha 2025/26

Ajouter un commentaire

HTML restreint

  • Vous pouvez aligner les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.
  • Vous pouvez légender les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.

About

MSD a été créée pour produire, acheter, stocker et distribuer les produits de santé approuvés nécessaires aux établissements de santé. Dans le cadre de cette mission, nous veillons à ce que les produits de santé en Tanzanie soient accessibles, fiables et abordables, et livrés à temps dans tous les établissements de santé en Tanzanie et au-delà.

Featured Posts

Contact info

Notre mission : Rendre les produits de santé de qualité accessibles à tous les établissements de santé publics en Tanzanie.