Aller au contenu principal
wishega

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala MSD, Ahimiza Watumishi Kutimiza Majukumu Yao

"Hakuna Haki Bila Wajibu" – Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala MSD, Ahimiza Watumishi Kutimiza Majukumu Yao. 

Katika kuendeleza uwajibikaji na ufanisi mahali pa kazi, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Mboyi Wishega, ametoa wito kwa watumishi wa taasisi hiyo kuzingatia wajibu wao kikamilifu ili kustahili haki zao zinazotolewa kwa mujibu wa taratibu na sheria za utumishi wa umma.

Akizungumza katika kikao kazi na madereva wa MSD, Bw. Wishega alisisitiza kuwa haki na wajibu ni dhana zinazokwenda pamoja, na kwamba haitarajiwi mtumishi kudai haki bila kutimiza wajibu wake ipasavyo.

"Hakuna haki bila wajibu! Hivi ni vitu viwili vinavyokwenda sambamba. MSD imeendelea kuwapatia watumishi wake haki zao kwa mujibu wa sheria, hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kuhakikisha anatimiza majukumu yake kwa uadilifu na weledi," alieleza Bw. Wishega.

Katika kikao hicho, kilicholenga kuhimiza uwajibikaji, nidhamu, na kutoa mrejesho kuhusu utendaji wa kazi, Bw. Wishega aliwataka madereva kuwa mfano wa kuigwa kwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia kanuni za usalama barabarani, utunzaji wa vyombo vya usafiri, pamoja na kuheshimu muda na maadili ya kazi.

Aidha, aliwahakikishia watumishi hao kuwa MSD itaendelea kuboresha mazingira ya kazi na kutoa haki zote stahiki ikiwa ni pamoja na mafao, likizo, bima za afya, na fursa za mafunzo – ilimradi wajibu pia utekelezwe kwa kiwango kinachotarajiwa.

Ajouter un commentaire

HTML restreint

  • Vous pouvez aligner les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.
  • Vous pouvez légender les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.

About

MSD a été créée pour produire, acheter, stocker et distribuer les produits de santé approuvés nécessaires aux établissements de santé. Dans le cadre de cette mission, nous veillons à ce que les produits de santé en Tanzanie soient accessibles, fiables et abordables, et livrés à temps dans tous les établissements de santé en Tanzanie et au-delà.

Featured Posts

Contact info

Notre mission : Rendre les produits de santé de qualité accessibles à tous les établissements de santé publics en Tanzanie.