Skip to main content
  • Rais Samia Afunga Kazi Sekta ya Afya - Wilaya ya Mvomero

    RAIS Dk.Samia Suluhu Hassan amefunga kazi Mvomero kwa serikali kukabidhi dawa na vifaa tiba vya zaidi ya sh. bilioni 1.61.

    Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Judithi Nguli wakati Bohari ya Dawa (MSD), ilipokabidhi dawa na vifaa tiba vya zaidi ya sh. bilioni 1.61 kwa vituo vya afya na hospitali za wilaya hiyo.

  • Serikali Kupitia MSD Kanda ya Dar es Salaam Yasambaza Vifaa Tiba vya Milioni 930 - Wilaya ya Ulanga.

    SERIKALI kupitia Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dar es Salaam imesambaza vifaa tiba vya zaidi ya sh. milioni 930 kwa ajili ya vituo vya afya 24 vya halmshauri ya Wilaya ya Ulanga.

    Akizungumza jana Wilayani humo mkoani  Morogoro Mbunge wa jimbo la Ulanga Salim Hasham, alisema, wamepokea vifaa tiba hivyo na dawa za zaidi ya sh. milioni 900 kwa ajili ya vituo vya afya 23 vya halmashauri ya Wilaya ya Ulanga.

  • Rais Samia Apeleka Tabasamu Kwa Wananchi wa Kata ya Magazini - Wilaya ya Namtumbo

    Kituo cha Afya cha Magazini kilichopo Kata ya Magazini  Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma  kimepata msaada wa vifaa Tiba vya kisasa vya upasuaji vikiwemo vya wamama wajawazito  vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 100 ili  kuweza kusaidia kuboresha huduma za afya kwenye kata hiyo, iliyoko mpakani na nchi ya msumbiji .

  • Changamoto za Usambazaji wa Dawa na Vifaa Tiba- Wilaya ya Ludewa

    Changamoto za jiografia zilizopo katika Wilaya ya Ludewa zimekuwa zikisababisha ugumu wa kufikisha dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya pamoja na kusafirisha wagonjwa hasa wanapopata rufaa kutoka vituo vya pembezoni kwenda Hospitali ya Wilaya.

    Hali hiyo inatokana na baadhi ya vijiji kuwepo katika miamba na vingine kwenye mwambao wa ziwa nyasa ambako hulazimika kusafiri majini kwa saa tatu mpaka kumi na mbili.

  • Serikali Yamwaga Vifaa Tiba vya Milioni 222.472 Mkoani Singida

    SERIKALI  ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Bohari ya Dawa (MSD) imekabidhi vifaa tiba Mkoa wa Singida vyenye jumla ya takribani Sh.Milioni 222.472, kwaajili ya kuboresha huduma za afya Mkoani humo.

    Vifaa hivyo ni pamoja na majenereta, sambamba na vifaa vitakavyotumika kuhudumia watoto wanaozaliwa kabla ya muda na huduma nyinginezo ambavyo vimekabidhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ikungi, Kituo cha Afya Sepuka na Hospitali ya Wilaya ya Singida, Ilongero.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.