MSD Yateta na Wazalishaji, Wasambazaji na Washitiri wa Bidhaa za Afya.
Bohari ya Dawa (MSD) imekutana na wazalishaji, wasambazaji na washitiri wa bidhaa za afya zaidi ya 200 kutoka nje na ndani ya nchi kujadiliana namna ya kuboresha ushirikiano na kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini.
Katika hafla hiyo Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewaeleza wadau hao kuwa serikali inaendelea kuboresha ushirikiano na sekta binafsi kuchagiza uanzishaji wa viwanda vya bidhaa za afya nchini.