MSD Kanda ya Mbeya, Yateta na Wafamasia Kuboresha Huduma
MBEYA:
MSD Kanda ya Mbeya imefanya kikao na wafamasia kutoka halimshauri 17 na wafamasia wa mikoa yote inayohudumiwa na Kanda hiyo
Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya Bw. Marco Masala amesema lengo la kikao hicho ni kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za upatikanaji wa bidhaa za afya katika mikoa hiyo, pamoja na kuimarisha uhusiano.
Pamoja na mambo mengine kupitia kikao hicho wamekubaliana kuunda kamati maalum ya kudumu itakayosaidiana na Kanda ya MSD Mbeya kufuatilia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa kwenye kikao hicho.