MSD Yaboresha Huduma za Kusafisha Damu- Hospitali ya Tumbi
PWANI
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani - Tumbi imeanza kutoa huduma mpya ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo. Huduma hii imeanza kutolewa baada ya Bohari ya dawa (MSD) kukamilisha usimikaji wa mashine za kisasa 10 za kusafisha damu, baada ya hospitali ya rufaa ya Tumbi kuboresha miundombinu ya kuwezesha huduma hiyo kupatikana.
Hatua hiyo ni muendelezo wa maboresho ya huduma za afya nchini yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Afya.