Skip to main content
  • Kanda ya MSD DSM Yakutana na Wateja Wake

    Wateja wa MSD kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya vilivyopo Mkoa wa Dar es Salaam leo wamepata fursa ya kutembelea ghala la kuhifadhia bidhaa za afya la Kanda ya Dar es Salaam na kujionea bidhaa mbalimbali zinazotunzwa na kusambazwa na MSD. Hatua hii imefanyika ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha wiki ya huduma kwa wateja. 

  • PSSSF Yaitambua MSD kama Mshirika Muhimu

    Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF umeitambua Bohari ya Dawa (MSD) kama mshirika muhimu katika kuchangia maboresho ya huduma za mfuko huo. Utambuzi huo umefanywa leo wakati wa hitimisho la wiki ya huduma kwa wateja. PSSSF imekuwa kwenye mahusiano mazuri ya kiutendaji na MSD hasa katika kuhakikisha michango ya watumishi wa MSD inawasilishwa PSSSF kwa wakati kwa kutumia mifumo mbalimbali ya kielektroniki. 

  • MSD Mtwara Yateta na Wadau Wake, Kuimarisha Huduma

    Katika kuhitimisha maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja, MSD Kanda ya Mtwara imefanya ziara maalum katika Kituo cha Afya Ufukoni kwa lengo la kukusanya maoni ya wateja na kujadili namna bora ya kuboresha huduma na mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya. Katika ziara hiyo, timu ya MSD Mtwara ilipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa kituo hicho pamoja na wananchi wanaonufaika na huduma zake, ili kusikiliza changamoto, matarajio na mapendekezo yao kuhusu huduma zinazotolewa na MSD.

  • MSD Iringa yajadili Maboresho ya Huduma na Wadau Wake, Yatunuku Zawadi

    Bohari ya Dawa (MSD) kupitia Kanda yake ya Iringa imetekeleza jukumu muhimu la kijamii kwa kukabidhi msaada wa vifaa tiba na zawadi mbalimbali kwa vituo vya kutolea huduma za afya katika mikoa ya Iringa na Njombe, ikiwa ni hitimisho la maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025.

    Miongoni mwa taasisi zilizopokea msaada mkubwa ni Hospitali ya Wilaya ya Wanging’ombe, ambapo MSD ilikabidhi zawadi mbalimbali kwa wadau hao, ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.

  • Kanda ya MSD Mwanza Kuboresha Huduma kwa Wateja Wake

    Kanda ya MSD Mwanza imekutana na wateja wake inaowahudumia ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja. Katika hafla hiyo mambo mbalimbali yalizungumzwa yakiwemo Kanda ya MSD Mwanza kuendelea kuboresha huduma zake lakini kuhakikisha mahusiano bora yaliyopo hivi sasa yanaendelea kuwepo.

    Kaimu Meneja Kanda ya Mwanza Masudi Lugandya amewashukuru wateja hao kwa kuitikia wito wa kuja kujumuika na watumishi wa kanda hiyo ili kutoa maoni yao lakini pia kusikiliza maoni kutoka MSD. 

About

MSD was established for the purpose of production, procurement, storage, and distribution of approved health commodities required for use by health facilities. In living this mission, we ensure that health commodities in Tanzania are accessible, reliable, and affordable but also delivered on time at all health facilities in Tanzania and beyond.

Featured Posts

Contact info

Our mission: To make quality health products accessible to all public health facilities in Tanzania.