Viongozi wa Sekta ya Afya Wahimizwa Kushirikiana na MSD
MOROGORO.
Wasimamizi na wadau wa afya mkoani Morogoro, wameaswa kushirikiana kwa ukaribu na Bohari ya Dawa (MSD), ili kwa pamoja waweze kutatua na kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya mkoani humo, kwa ajili ya ustawi watu na maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Rai hiyo imetolewa hii leo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wà Morogoro, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini Mhe. Rebeka Nsemwa, wakati akifungua kikao kazi cha wateja na wadau wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, kilichokutanisha viongozi wa sekta ya afya ngazi ya mkoa na wilaya mkoani humo.