Sisi ni nani
Bohari ya Dawa (MSD) ni taasisi inayojiendesha inaofanya kazi chini ya Wizara ya Afya (MoH) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ilianzishwa mwaka 1993 kwa kupitishwa kwa Sheria ya Idara ya Bohari ya Dawa, Sura ya 70. Mwaka 2021, Sheria ilifanyiwa marekebisho ili kupanua mamlaka ya MSD kwa kuongeza uzalishaji wa ndani wabidhaa za afya kwenye kazi zake kuu. Leo, MSD imekabidhiwa jukumu la uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya kwa vituo vya afya vya umma kote nchini.
Bodi ya Wadhamini hutumika kama mamlaka ya juu zaidi ya kufanya maamuzi kwa MSD. Inawajibika kwa utawala, mwelekeo wa kim-
kakati, na uangalizi kwa niaba ya Wizara ya
Afya.
Bodi ina wajumbe tisa (9), walioteuliwa kwa muda wa miaka mitatu. Mwenyekiti anateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wajumbe wanane (8) waliobaki wanateuliwa na Waziri wa Afya. Mkurugenzi Mkuu wa MSD anakaimu nafasi ya Katibu wa Bodi lakini hana haki ya kupiga kura