Skip to main content

MSD yaendelea kutoa elimu kupitia maonyesho

Bohari ya Dawa (MSD) inashiriki katika maonesho ya kimataifa ya bidhaa za Afya (Medexpo) yanayofanyika jijini Dar es Salaam. Lengo la maonyesho hayo ni kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya kutoka ndani na nje ya nchi.

MSD ikiwa mmoja wa wadau wakubwa kwenye sekta ya afya inashiriki maonesho hayo kwa kutoa elimu kwa wadau kuhusu namna ya kushiriki kwenye zabuni zinazotangazwa na MSD kupitia mfumo wa Nest, pamoja na kuwajengea uelewa wadau juu ya sheria na taratibu za ununuzi wa umma.

Aidha, wananchi na wadau mbalimbali wa MSD wamepata wasaa wa kujionea bidhaa za afya mbalimbali zinazozalishwa na zinazosambazwa na MSD kwenye vituo vya kutolea hufuma za afya. Bidhaa hizo ni pamoja na vifaa tiba, dawa na vitendanishi vya maabara.

Add new comment

Restricted HTML

  • You can align images (data-align="center"), but also videos, blockquotes, and so on.
  • You can caption images (data-caption="Text"), but also videos, blockquotes, and so on.

About

MSD was established for the purpose of production, procurement, storage, and distribution of approved health commodities required for use by health facilities. In living this mission, we ensure that health commodities in Tanzania are accessible, reliable, and affordable but also delivered on time at all health facilities in Tanzania and beyond.

Featured Posts

Contact info

Our mission: To make quality health products accessible to all public health facilities in Tanzania.