Changamoto za Usambazaji wa Dawa na Vifaa Tiba- Wilaya ya Ludewa
Changamoto za jiografia zilizopo katika Wilaya ya Ludewa zimekuwa zikisababisha ugumu wa kufikisha dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya pamoja na kusafirisha wagonjwa hasa wanapopata rufaa kutoka vituo vya pembezoni kwenda Hospitali ya Wilaya.
Hali hiyo inatokana na baadhi ya vijiji kuwepo katika miamba na vingine kwenye mwambao wa ziwa nyasa ambako hulazimika kusafiri majini kwa saa tatu mpaka kumi na mbili.