Skip to main content
  • MSD na Wadau wa Afya Mkoa wa Dar es Salaam Wahimizwa Kushirikiana

    Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Bi.Rehema Madenge, amewataka wadau wa afya mkoani humo, kushirikiana kwa karibu na Bohari ya Dawa (MSD) ili kuboresha huduma na kutatua changamoto mbalimbali zinazoukabili mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya mkoani humo. 

  • Mtendaji Mkuu Global - Fund, Atembelea MSD

    Dar es Salaam.

    Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Dunia (Global fund) Bw. Peter Sands, amefanya ziara Bohari ya Dawa (MSD) na kujionea namna MSD inavyotekeleza majukumu yake.

    Kupitia ziara hiyo, Mtendaji Mkuu huyo, amepata wasaa wa kutembelea maghala ya kuhifadhia bidhaa za afya, yanayomilikiwa na MSD, yaliyoko Keko, jijini Dar es Salaam.

    Bwana Sands ameahidi kuwa mfuko huo utaendelea  kuiwezesha MSD kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya, hasa za miradi Msonge, huku akiipongeza MSD kwa kufanikisha usambazaji wa vyandarua nchini.

  • Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Atoa Rai kwa Watumishi wa Afya

    Singida.

    Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatma Mganga, ametoa rai kwa MSD na wataalamu wengine wa afya wakiwemo Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaboresha huduma kwenye maeneo yao, ikiwemo upatikanaji wa bidhaa za afya, ili kuwahudumia wananchi kwa utimilifu.

    Dkt. Mganga ametoa rai hiyo leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD na Wadau wake, kilichofanyika Mkoani Singida.

  • MSD Yapongezwa Kuanzisha Mikutano na Wadau Wake

    Dodoma.

    Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Ally Senga Gugu, ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dodoma kwa kukutana na wadau wake na kujadili masuala mbalimbali yahusuyo mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, yanayogusa pande zote mbili kwa lengo la kuboresha huduma na kuleta tija kwa wananchi. 

  • Mhe. Queen Sendiga Aipongeza MSD.

    Rukwa.

    Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga amefurahishwa na huduma za MSD Mkoani humo na kusema kwamba hivi sasa huduma za afya hasa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika kwa kiasi kikubwa.

    Mhe. Sendiga ameongeza kuwa huduma na uhusiano wa MSD na Uongozi wa Mkoa wa Rukwa umeimarika na kwamba kero mbalimbali zilizokuwepo hapo awali, mathalani za upungufu wa bidhaa za afya sasa zimetatuliwa kwa kiasi kikubwa.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.