Serikali Yakabidhi Vifaa Tiba vya Mil. 200 Mkoani Njombe
Serikali Kupitia Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Iringa imekabidhi vifaa tiba katika kituo cha afya cha Kifanya Halmashauri ya Mji wa Njombe mkoani humo vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 200.
Kituo hicho cha afya ni kati ya vituo vipya vilivyojengwa na serikali hivi karibuni lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi.
Akizungumza mwishoni mwa wiki Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Robert Lugembe, alisema hatua hiyo ni katika kuunga mkono juhudi za serikali ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za afya.