Skip to main content
  • Serikali Yakabidhi Vifaa Tiba vya Mil. 200 Mkoani Njombe

    Serikali Kupitia Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Iringa imekabidhi vifaa tiba katika kituo cha afya cha Kifanya Halmashauri ya Mji wa Njombe mkoani humo  vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 200.
     
    Kituo hicho cha afya ni kati ya vituo vipya vilivyojengwa na serikali hivi karibuni lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi.
     
    Akizungumza mwishoni mwa wiki Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Robert Lugembe, alisema hatua hiyo ni katika kuunga mkono juhudi za serikali ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za afya.
     

  • Dkt. Philip Mpango Aweka Jiwe la Msingi Kiwanda cha Mipira ya Mikono cha MSD, Kilichopo Idofi Makambako Mkoani Njombe

    Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amesema serikali inatambua vita iliyopo katika ujenzi wa viwanda vya dawa lakini kwa kuwa uwamuzi huo ni wa Rais Dk. Samia Suluhi Hassan hakuna atakayefanikiwa kuvikwamisha hivyo vitajengwa.

    Amesema kwa sasa  serikali inaagiza dawa kwa asilmia 80 na vifaa tiba kwa asilimia 90 kutoka nje ya nchi, hali inayosababisha uhaba wa vifaa na gharama kubwa za uagizaji wa vifaa vya afya  hivyo ni lazima kuchukua maamuzi magumu.

  • Rais Dkt. Samia Analeta Mapinduzi Viwanda vya Dawa

    WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amedhamiria kuleta mapinduzi katika sekta ya viwanda hasa vya dawa, vifaa tiba.

    Rais Dkt. Samia ameendelea kutoa fedha za uwekezaji katika sekta ya viwanda na miradi yote ya maendeleo iliyoanzishwa awamu ya tano inatekelezwa.

    Mwalimu aliyasema hayo mkoani Njombe wakati akikagua uzalishaji katika kiwanda cha mipira ya mikono (gloves) kilichopo Idofi, mkoani humo.

  • Upatikanaji wa Dawa nchini, Wapaa hadi Kufikia 81%

    Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa nchini (MSD), Mavere Tukai amesema kuwa upatikanaji wa dawa nchini umefikia asilimia 81 mwezi Juni 2023 kutoka asilimia 57 mwezi Juni 2022 jambo ambalo limechangia kurahisisha utoaji huduma nchini.

    Ameyasema hayo Septemba 27, 2023 jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi na wahariri wa vyombo vya habari nchini chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

  • MSD Yazindua Kampeni ya Usambazaji Vyandarua Ngazi ya Kaya - Mkoa wa Tabora

    MKOA wa Tabora umetajwa kuwa wa kwanza kitaifa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa wa malaria hali inayotokana na imani potofu ya matumizi ya vyandarua vyenye dawa kuwa vinapunguza nguvu za kiume.

    Takwimu zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa malaria kimeongezeka kutoka asilimia 11.7 mwaka 2016/2017 hadi asilimia 23.4 mwaka 2022 wakati kiwango cha maambukidhi ya malaria kitaifa ni asilimia 8.1.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.