Skip to main content
  • Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na UKIMWI Yaridhishwa na Utendaji wa MSD.

    Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imesema  imeridhishwa na hali ya utendaji wa Bohari ya Dawa(MSD) na mipango ya utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo uzalishaji wa dawa ili kupunguza kununua dawa nje ya nchi. 

    Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stansilaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya hali ya utendaji na majukumu ya Bohari ya Dawa (MSD), ambapo ameichagiza MSD kuongeza ufanisi, ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha bidhaa za afya zinakuwa toshelevu na  kusambazwa.

  • MSD Yaanza Usambazaji wa Vifaa Tiba kwa Majimbo ya Mkoa wa Morogoro

    BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza usambazaji majimboni vifaa  tiba  vilivyonunuliwa na serikali vyenye  thamani ya zaidi ya Sh bilioni 14.9 kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati  lengo ni kupunguza vifo vya mama na mtoto.

    Meneja wa MSD, Kanda ya Dar es salaam, inayohudumia mikoa ya  Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Visiwa vya Zanzibar, Betia Kaema alisema hayo wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Adam Malima kwa ajili ya majimbo 11 ya Mkoa huo.

  • Rais Samia Atoa Vifaa Tiba vya Mil. 691 Kwa Majimbo 10 - Dar es Salaam

    RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hususani huduma ya mama na mtoto lengo likiwa ni kupunguza vifo vitonavyo na uzazi pingamizi.

    Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alipokuwa akiwakabidhi wabunge wa majimbo 10 ya mkoa wa Dar es Salaam, vifaa tiba vyenye thamani ya sh. Milioni 691 vilovyotolewa na serikali kwa majimbo hayo.

  • Waziri Ummy Azindua Usambazaji wa Vifaa Tiba vya Huduma za Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto

    Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu azindua usambazaji wa vifaa vya kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto vya zaidi ya sh.bilioni 14.9 ambavyo vitasambazwa katika majimbo 214 na halmashauri nchi nzima.

    Akizungumza jijini Dar es Salaam Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa uzinduzi huo, Waziri Ummy alisema uzinduzi wa usambazaji wa vifaa vya hivyo umelenga kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto na kuimarisha uzazi salama nchini.

  • Katibu Mkuu Afya, Aitaka MSD Kuwajali Wateja Wake

    Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. John Jingu ameilekeza Bohari ya Dawa (MSD) kuwajali wateja na kuwashirikisha katika suala zima la kuwapa huduma za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za Afya nchini.

    Dkt. Jingu amesema hayo wakati  akifungua kikao cha ishirini na mbili  (22) cha baraza la Wafanyakazi la MSD Mkoani Morogoro ambapo amesisitiza kuwa, kujali wateja ni msingi wa kuwahudumia kulingana na mahitaji yao.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.