Skip to main content
  • MSD Yasambaza Vifaa Tiba vya Kisasa Wilayani Mafia

    BOHARI ya Dawa (MSD) imesema usambazaji wa dawa na vifaa vya kisasa Kisiwani Mafia mkoani Pwani umefanikiwa kupunguza rufaa za wagonjwa kutoka kisiwani humo kwenda kutibiwa jijini Dar es Salaam.

    Akizungumza jana kisiwani Mafia Afisa Huduma kwa Wataeja wa MSD wa kanda hiyo Diana Kimario, alisema Bohari hiyo imefanikiwa kupunguza rufaa za wagonjwa kutoka kisiwani Mafia kwenda jijini Dar es Salaam kwa kufunga vifaa tiba vya kisasa hususani vya maabara na upasuaji.

  • MSD Yateta na Wazalishaji, Wasambazaji na Washitiri wa Bidhaa za Afya.

    Bohari ya Dawa (MSD) imekutana na wazalishaji, wasambazaji na washitiri wa bidhaa za afya zaidi ya 200 kutoka nje na ndani ya nchi kujadiliana namna ya kuboresha ushirikiano na kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini.

    Katika hafla hiyo Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewaeleza wadau hao kuwa serikali inaendelea kuboresha ushirikiano na sekta binafsi kuchagiza uanzishaji wa viwanda vya bidhaa za afya nchini.

  • MSD Mfano wa Kuigwa SADC

    Wakuu wa Taasisi za Bohari ya Dawa pamoja na viongozi wanaosimamia manunuzi ya bidhaa za afya katika  Jumuia ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wameeleza kuwa Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) imekuwa mfano wa kuigwa katika nchi za jumuiya hiyo.

    Aidha wamesema MSD itakuwa chachu ya kuunganisha maendeleo na kukuza uchumi wa Afrika kutokana na ufanisi wake katika  upatikanaji wa uhakika wa dawa na bidhaa za afya.

  • Wafamasia na Wataalamu wa Maabara Nchini, Waaswa Kuzingatia Wajibu Wao

    Wafamasia na Wataalamu wa Maabara Kanda ya Kagera wametakiwa kutambua moyo wa sekta ya afya uko katika upatikanaji wa dawa na vifaa tiba na kwamba kuhakikisha bidhaa hizo hazikosi katika vituo vya kutolea huduma.

  • MSD Kuja na Suluhu ya Special Procurement

    Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, ambaye pia ni mlezi wa Kanda ya MSD Kagera Bi. Rosemary Slaa, amewahakikishia wataalamu wa afya kutoka Mikoa ya Kagera na Geita kuwa Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea kufanya maboresho katika upatikanaji wa bidhaa za afya nchini, mathalani upatikanaji wa vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa wakati.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.