Skip to main content
atibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Ally Fatma Mganga (Aliyesimama), Akihutubia Wakati wa Kikao cha MSD na Wadau Wake Kutoka Mkoa wa Singida

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Atoa Rai kwa Watumishi wa Afya

Singida.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatma Mganga, ametoa rai kwa MSD na wataalamu wengine wa afya wakiwemo Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaboresha huduma kwenye maeneo yao, ikiwemo upatikanaji wa bidhaa za afya, ili kuwahudumia wananchi kwa utimilifu.

Dkt. Mganga ametoa rai hiyo leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD na Wadau wake, kilichofanyika Mkoani Singida.

Ameongeza kuwa serikali ya Awamu ya Sita imejenga vituo vingi vipya vya kutolea huduma za afya nchini na kuviongeza hadhi vingine, hivyo kazi kubwa kwa MSD ni kuhakikisha bidhaa za afya hitajika katika vituo hivyo zinapatikana kwa wakati na huduma za afya zinatolewa kwa wananchi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victoria Ludovick, ameipongeza MSD kwa kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya Mkoani humo, ambapo kwa sasa umefikia asilimia 88%.

Hata hivyo, ameisihi MSD kuendelea kuboresha upatikanaji huo ili uwe maradufu, mathalani upatikanaji wa vifaa tiba.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma. Bw. John Sipendi, amewashukuru wadau hao kwa kuitia mualiko huo, huku akihimiza umuhimu wa mijadala ya wazi ili kupata suluhu ya changamoto mbalimbali na hatimae kutoka na maazimio ambayo yatasaidia kuboresha huduma kwa pande zote mbili.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.