Skip to main content
Wajumbe Kutoka Bohari ya Dawa (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) Msumbiji, Wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Uongozi wa Bohari ya Dawa (MSD), Mara Baada ya Kutembelea Makao Makuu ya MSD Kwa Lengo la Kubadilishana Uzoefu.

Bohari ya Dawa Msumbiji Yapongeza Juhudi za MSD Kuboresha Huduma, Pamoja na Ujenzi wa Viwanda

Ujumbe kutoka Bohari ya dawa (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) Msumbiji leo wametembelea MSD Makao Makuu kwa lengo la kujifunza na kubadirishana uzoefu.

 Ujumbe huo Msumbiji ulifanya ziara ya kutembelea maghala ya kuhifadhia bidhaaza afya ya MSD pamoja na kiwanda cha kuzalisha barakoa na kiwanda cha kuzalisha vidonge KPI.

Ujumbe huo umevutiwa na hatua ya MSD kuongeza jukumu la kuzalisha bidhaa za afya ambazo zinasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza Gharama za kuagiza bidhaa hizo kutoka nje.

Aidha, pamoja na mambo mengine ujumbe huo ulikutana na Kurugenzi za Ugavi na TEHAMA na kupata maelezo namna mifumo mbalimbali inavyofanya kazi katika mnyororo wa ugavi na kuahidi kuiga mazuri punde tu warejeapo nchini kwao.

Katika hatua nyingine ujumbe huo ulipata fursa ya kutembelea wateja wa MSD ambao ni hospitali ya Mifupa, MOI na Taasisi ya Moyo (JKCI) kwa lengo la kujifunza namna taasisi hizo zinavyoendesha shughuli zake.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.