Aller au contenu principal

MSD yafanya kikao na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC),

Bohari ya Dawa (MSD) leo imefanya kikao muhimu na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Mheshimiwa Elias M. Magosi, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa SADC, kikao hiko kiliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, kilikuwa na lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya afya.

Katika kikao hicho, pande zote mbili zilijadiliana kuhusu mikakati ya pamoja ya kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya ndani ya ukanda wa SADC, kuongeza usalama wa bidhaa za afya, pamoja na kushirikiana katika maeneo ya uzalishaji, utafiti, na usambazaji wa dawa.

Akizungumza katika kikao hicho, Mavere Tukai, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, alieleza dhamira ya taasisi hiyo kushirikiana na nchi wanachama wa SADC kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa bora za afya kwa gharama nafuu. “Tunaamini kuwa kupitia ushirikiano huu wa kikanda, tutaongeza uwezo wa pamoja wa kiutendaji, kuongeza ufanisi wa manunuzi na kurahisisha usambazaji wa dawa na vifaa tiba kwa wananchi wetu,” alisema Tukai.

Aidha kwa upande wake, Mheshimiwa Elias M. Magosi alipongeza juhudi za MSD katika kuhakikisha huduma bora za afya nchini na kueleza kuwa mafanikio hayo yanatoa mfano bora kwa nchi nyingine wanachama wa SADC. “MSD imeonyesha kiwango cha juu cha uwajibikaji, ubunifu, na weledi—na kwa kweli ni taasisi ya kuigwa ndani ya ukanda wa SADC. Tunaipongeza kwa mafanikio haya na tuna matumaini makubwa ya kuimarisha ushirikiano wetu katika kuleta mageuzi chanya kwenye sekta ya afya kwa nchi wanachama,” alisema Magosi.

 

Ajouter un commentaire

HTML restreint

  • Vous pouvez aligner les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.
  • Vous pouvez légender les images (data-align="center"), mais également les vidéos, citations, etc.

About

MSD a été créée pour produire, acheter, stocker et distribuer les produits de santé approuvés nécessaires aux établissements de santé. Dans le cadre de cette mission, nous veillons à ce que les produits de santé en Tanzanie soient accessibles, fiables et abordables, et livrés à temps dans tous les établissements de santé en Tanzanie et au-delà.

Featured Posts

Contact info

Notre mission : Rendre les produits de santé de qualité accessibles à tous les établissements de santé publics en Tanzanie.