Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Aonya Matumizi Mabaya ya Vyandarua
#SONGWE
MKUU wa Mkoa wa Songwe, Dk. Francis Michael, ameonya matumizi mabaya ya vyandarua kama vile kufugia kuku au kuvulia samaki.
Akizungumza jana mkoani humo wakati akizinduza mpango wa ugawaji wa vyandarua katika shule za msingi Dk.Micheal amesisitiza kuwa vitendo hivyo vinaathiri juhudi za Serikali na wadau wa afya katika kupambana na Malaria.