Aller au contenu principal
  • SADC Yazindua Kanzidata ya Mfumo wa Taarifa za Bidhaa za Afya Kwa Nchi Wanachama.

    Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) imezindua Kanzidata maalumu kwaajili ya ukusanyaji na uchakataji wa taarifa za Dawa na vifaa tiba kutoka kwa wazalishaji na wazabuni mbalimbali Duniani, ambapo mfumo huo utarahisisha upatikanaji na ununuzi wa bidhaa za afya kutoka kwa nchi wanachama.

  • Wataalamu wa Afya Kutoka Sierra Leone, Wafanya Ziara ya Mafunzo MSD

    Wataalamu wa Afya kutoka nchini Sierra Leone leo wametembelea Bohari ya Dawa (MSD) kwa lengo kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu shughuli za Ugavi, Uhifadhi, Uendeshaji, Ununuzi, Huduma kwa Wateja, Sera, Udhibiti Ubora, pamoja na mambo mengine yanayohusu mnyororo wa Ugavi wa bidhaa za afya.

    Akiongea kwa niaba ya Wizara ya Afya wakati wa kuukaribisha ujumbe huo nchini, Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi, amesema ujio wa wageni hao ni ishara kwamba kama nchi tumeboresha na kuimarisha Bohari yetu katika utoaji wa huduma, ndio maana wengine wanakuja kujifunza.

  • Somalia Kushirikiana na MSD, Ununuzi wa Bidhaa za Afya

    Rais wa Somalia Mheshimiwa Hassan Sheikh Mohamud amesema nchi yake imeamua kushirikiana kwa karibu na Bohari ya Dawa ya Tanzania katika ununuzi wa bidhaa za afya na kubadilishana uzoefu wa namna mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya unavyofanya kazi.

    Rais Mahamud ambaye yuko ziarani nchini Tanzania, ameyasema hayo alipoitembelea MSD, na kuongeza kuwa kutokana na uzoefu wa MSD, wana uhakika kuwa ubora wa bidhaa za afya utakuwa wa uhakika.

  • Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aipongeza MSD kwa Maboresho ya Huduma

    Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameupongeza uongozi wa Bohari ya Dawa (MSD) kwa mabadiliko makubwa yanayoendelea katika taasisi hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa yamewezesha kupunguza malalamiko ya uhaba wa bidhaa za afya nchini, mathalani malalamiko ya uhaba wa dawa.

    Mhe. Senyamule ameeleza kwamba awali wakienda kwenye mikutano ya hadhara kuongea na wananchi, walikumbana na malalamiko mengi ya uhaba wa dawa, lakini hivi karibuni hali imebadilika, japokuwa bado kuna changamoto, lakini angalau inatia moyo kuona kuna mageuzi yanafanyika.

  • MSD KUSAMBAZA VIDONGE MIL. 22 VYA VITAMINI A NCHINI

    Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameikabidhi Serikali ya Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu vidonge milion 22  vya matone vya Vitamini A kwa ajili ya watoto, vilivyotolewa na serikali ya Canada, kupitia shirika la Nutrition International (NI). 

    Dkt. Kikwete, amekabidhi dawa hizo akiwa mmoja wa wajumbe wa bodi wa Shirika la kimataifa la Nutrition international ambalo ndio limetoa msaada huo. 

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.