SADC Yazindua Kanzidata ya Mfumo wa Taarifa za Bidhaa za Afya Kwa Nchi Wanachama.
Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) imezindua Kanzidata maalumu kwaajili ya ukusanyaji na uchakataji wa taarifa za Dawa na vifaa tiba kutoka kwa wazalishaji na wazabuni mbalimbali Duniani, ambapo mfumo huo utarahisisha upatikanaji na ununuzi wa bidhaa za afya kutoka kwa nchi wanachama.