Skip to main content
Maafisa Kutoka MSD, (wa kwanza kushoto, na wapili kulia), Wakikabidhi Nyaraka za Vifaa Tiba kwa Uongozi Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es salaam

MSD Yakabidhi Vifaa Tiba vya Mil. 500 - Hospitali ya Wilaya Kisemvule

SERIKALI  kupitia Bohari ya Dawa (MSD), imekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 500 kwa hospitali ya Wilaya ya Ilala (Kivule), lengo ni kuboresha hali ya utoaji huduma wilayani humo.

Vifaa hivyo ni pamoja na Vitanda vya kulalia wagonjwa, ventileta za ICU, viti mwendo, friji za kuhifadhia damu na sampuli, vitanda vya uchunguzi, Sunction machine, Ultra Sound machine, magodoro na mashuka.

Akizungumza wakati wa kupokea vifaa hivyo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dk. Zaituni Hamza, ameishukuru serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa ujio wa vifaa hivyo, kwani vinaakisi adhma na dhamira ya kuboresha huduma za afya nchini.

Aliongeza kuwa, huduma za mama na mtoto kwasasa zimeboreka kuliko wakati mwingine wowote, hali ambayo inasababisha kupungua kwa vifo vya wajawazito na watoto wachang wakati wa kujifungua.

Katika hatua nyingine, alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai, kwa maboresho ya huduma, ambapo kwa sasa zimeimarika, mawasiliano yameboreshwa kati ya bohari na wateja wake hali inayosababisha hospitali kupata msaada wa haraka pale wanapokua na uhitaji.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.